Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, April 3, 2018

Simba SC kuchuana na Njombe Leo


Mtanange wa kiporo cha Ligi Kuu Bara uliokuwa unasubiriwa kwa hamu kati ya Njombe Mji dhidi ya Simba SC unapigwa leo Sabasaba Stadium.

Simba inaingia kucheza mechi hiyo baada ya awali kusogezwa mbele ili kuipa nafasi ya kujiandaa na mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Al Masry SC.

Kuelekea mechi hii, Simba inaweza ikamkosa mchezaji wake, kiungo Jonas Mkude, aliyeumia kifundo cha mguu japo siku mbili zilizopita alianza mazoezi mepesi chini ya unagalizi wa daktari, Yassin Gembe.

Endapo Simba wataibuka washindi katika mchezo huo, watazidi kuipa kisogo Yanga kwa kufikisha alama 49 dhidi ya 46 za Yanga iliyo nafasi ya pili.

Mara ya mwishi timu hizi zilipokutana, Simba ilishinda kwa jumla ya mabao 4-0 kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment