Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, March 11, 2018

Tillerson asitisha shughuli alizopanga kufanya Kenya leo baada ya kuugua

Tillerson augua nchini Kenya

Haki miliki ya pichaAFP
Image captionTillerson augua nchini Kenya
Waziri wa mambo nje wa Marekani, Rex Tillerson amesitisha shughuli alizokuwa anapaswa kufanya nchini Kenya kutokana na hali yake ya kiafya kutokuwa nzuri.

Msemaji wake amesema,Tillerson amekuwa kwenye ratiba ngumu katika ziara yake ya Afrika wakati huo huo akitumia muda mwingi kwenye mazungumzo ya simu kufuatilia kazi nyingine nchini mwake kama vile suala la Korea Kaskazini.
KenyattaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTillerson alipokutana na rais Uhuru Kenyatta
Maasifa wamesema watahairisha baadhi ya ratiba ambazo bwana Tillerson alikuwa ameweka ikiwa ni pamoja na safari yake ya kwenda kuona eneo ambalo ubalozi wa Marekani ulikuwa umelipuliwa mwaka 1998.
Rex Tillerson amekuwa katika ziara ya mataifa matano ya Afrika tangu siku ya jumatano akiwa ameanzia Ethiopia na sasa yuko Kenya kwa siku ya pili.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment