Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, March 11, 2018

Rais pekee mwanamke Afrika kujizulu kwa tuhuma za ubadhilifu

Rais wa Mauritian Ameenah Gurib-Fakim

Haki miliki ya pichaAFP
Image captionRais wa Mauritian Ameenah Gurib-Fakim
Rais wa Mauritian Ameenah Gurib-Fakim amekubali kuachia madaraka baada ya kutuhumiwa kutumia kadi ya benki yenye thamani ya dola za kimarekani elfu kumi iliyotolewa na shirika la msaada katika matumizi yake binafsi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Reuters,rais huyo amekana kosa hilo na kudai kuwa alirudisha fedha zote.
Rais huyo aliyeingia madarakani mwaka 2015 alikuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa nchini Mauritius.ambaye alikuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kwenye madhimisho ya Marais wa Mauritus.
Waziri mkuu wa nchi hiyo Pravind Jugnauth amewaambia waandishi wa habari kuwa rais Ameenah ataachia wadhifa wake kama ilivyopanga na kuongeza kwa kusema kuwa kipaumbele cha taifa hilo ndio kilichozingatiwa ili taifa hilo liendele kuwa nchi ya mfano.
Hata hivyo gazeti moja nchini humo lilichapisha uthibitisho wa nakala ambazo rais huyo alifanyia manunuzi ya vitu vyake vya thamani nchini Uingereza.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment