Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, March 2, 2018

Rais Emmerson avutia wawekezaji

Rais Emmerson Mnangagwa amewataka wawekezaji nchini Zimbabwe wasiwe na wasiwasi kuhusu hali isiyotabirika ya kisiasa kutokana na uchaguzi mkuu utakaofanyika katikati ya mwaka huu.

Rais Mnangagwa amesema Zimbabwe ni nchi ya amani, na anakaribisha nchi zote kufanya biashara na nchi yake katika mazingira ya amani.

Ameongeza kuwa serikali ya Zimbabwe itahakikisha uchaguzi mkuu unafanyika kwa uhuru, haki na kuaminika, kwa kulingana na kanuni za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC na Umoja wa Afrika.

Amesema serikali ya Zimbabwe inajiandaa kuhimiza mageuzi ya kiuchumi, ili kuongeza uwezo wa ushindani wa nchi hiyo, na kuifanya Zimbabwe iwe nchi inayovutia zaidi uwekezaji barani Afrika.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment