Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, February 25, 2018

Muhimbili yafanikiwa kuweka rekodi kubwa leo

Hospitali ya Taifa Muhimbili imewawashia vifaa vya usikivu watoto sita waliofanyiwa upasuaji maalumu wa kupandikiza vifaa vya usikivu, hatua ambayo leo hii imewawezesha watoto hao kwa mara ya kwanza kusikia sauti tangia wazaliwe.

Daktari wa upasuaji Pua, Koo na Masikio Dkt. Edwin Liyombo, amesema kuwashwa kwa vifaa hivyo kunaifanya hospitali ya Taifa Muhimbili kuwa na uwezo wa kufanya upasuaji wa kupandikisha vifaa vya usikivu, upasuaji ambao umekuwa unafanyika nje ya nchi tena kwa gharama kubwa.

Kwa upande wake, mwakilishi wa kampuni inayotengeneza vifaa hivyo ambaye pia ni daktari bingwa wa masuala ya sauti na upandikizaji vifaa vya usikuvu Dkt. Fayaz Jaffer, amesema itachukua takribani mwaka mmoja hadi watoto hao waweze kuzungumza ipasavyo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment