Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, February 26, 2018

Gesi ya Klorini yatumiwa Syria


Waathiriwa wa mashambulizi Syria
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWaathiriwa wa mashambulizi Syria
Maafisa wa Afya nchini Syria katika maeneo ya waasi yaliyozingirwa kaskazini mwa Ghouta wamesema watu kadhaa wamedhurika kutokana na na dalili zinazoonesha kuathiriwa na gesi ya Klorini, wakati wa mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na majeshi yanayounga mkono serikali.
Taaarifa uiliyotolewa na Wizara ya Afya inayoendeshwa na wapinzani imesema waathirika, madereva wa magari ya kubeba wagonjwa na watu wengine wameripotiwa kuvuta gesi hiyo ya Klorini baada ya mlipuko.
Watu 18 wanatibiwa kwa kuwekewa Oxygen.
Mkazi mmoja katika eneo la mashariki ya Ghouta ameiambia BBC kuna mtoto pia ameathirika.
Dokta Mohammed Khatoub aliyeko Uturuki, ambaye anatokea katika mji wa Ghouta ameelezea uthibitisho wa hospital wanakotibiwa majeruhi hao, kwamba wameathiriwa na gesi hiyo.
Hata hivyo Serikali ya Syria siku zote imekuwa ikikanusha kutumia silaha za kemikali.
Mashambulizi ya ardhini yalipamba moto jana Jumapili, licha ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutaka kusimamishwa kwa mapigano hayo.
BBC
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment