SERIKALI wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa imetoa tahadhari kwa wakazi wa wilaya hiyo kutokana na kuwapo kwa mlipuko unaodhaniwa kuwa ni homa ya uti wa mgongo.
Mkuu wa wilaya hiyo, Dk. Khalfan Haule, alitoa tahadhari hiyo jana akisema kuwa tayari kumeripotiwa kuwapo kwa homa inayodhaniwa kuwa ni ya ugonjwa wa uti wa mgongo kwenye kijiji cha Tentula na Kianda Kata ya Ikozi Sumbawanga Vijijini na kuwa mpaka sasa watu watatu wameugua na mmoja kufariki dunia kwa ugonjwa huo.
Kaimu Mganga Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Emmanuel Mtika, alisema ametuma timu ya wataalamu wa afya ili wafanye uchunguzi wa taarifa hizo katika vijiji hivyo.
Alisema kwa upande wa wagonjwa waliolazwa nao wanaendelea na matibabu, lakini vipimo havijatolewa ili kuthibitisha, lakini alitoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari katika kuepuka ugonjwa huo pamoja na magonjwa mengine.
No comments
Post a Comment