Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, February 2, 2017

Kiongozi wa upinzani DRC Etienne Tshisekedi afariki dunia



Tshisekedi alikuwa kiongozi maarufu wa upinzani kwa miongo kadhaa

Image captionTshisekedi alikuwa kiongozi maarufu wa upinzani kwa miongo kadhaa
Kiongozi wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Etienne Tshisekedi, amefariki dunia mjini Brussels nchini Ubelgiji akiwa na umri wa miaka 84.
Tshisekedi alikwenda mjini Brussels mwishoni mwa mwezi jana kwa ajili ya matibabu.
Bwana Tshisekedi alikuwa mmoja wa wanasiasa wakongwe waliokuwa mstari wa mbele kupigania demokrasia ya nchi yake.
Tshisekedi alikuwa na mvuto mkubwa kwa wananchi wa DRC
Image captionTshisekedi alikuwa na mvuto mkubwa kwa wananchi wa DRC
Alisimama kidete katika utawala wa aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Rais Mobutu Sese Seko, ambae utawala wake ulidumu kwa miongo kadhaa kabla ya kupinduliwa.
Etienne Tshisekedi pia alikuwa mpinzani wa Rais Laurent Kabila, ambae aliingia madarakani mnamo mwaka 1997, na mwanae, Rais Joseph Kabila, ambae hivi sasa ndio anatawala nchi hiyo.
Habari  kwa hisani ya BBC Swahii
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment