Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, January 25, 2017

IDADI YA WALIOKUFA AJALI YA BASI LA VITU LAINI NA LORI IRINGA YAONGEZEKA .


IDADI ya  vifo vya ajali ya basi la  kampuni Vitu laini lenye namba za usajili T910 linalofanya safari zake kati ya Lulanzi wilaya ya  Kilolo  na Iringa mjini  kufeli breki na  kuligonga lori lenye namba T724 AVV scania lililobeba Mbao jana eneo la Tagamenda Iringa mjini imeongezeka   kufikia  watu  wawili baada majeruhi mmoja  Neema Fungo (37) mkazi wa Ndiwili Iringa kufariki dunia wakati  akipatiwa matibabu . .


Mtandao  huu wa matukiodaimaBlog umefika Hospitali ya  Rufaa ya  mkoa  wa Iringa  na  kuzungumza na uongozi  wa Hospitali  hiyo leo 

 Muunguzi mfawidhi  msaidizi wa Hospitali ya  Rufaa ya  mkoa  wa Iringa Victoria Ntara  alisema walipokea majeruhi 52 wa  ajali  hiyo  iliyotokea  eneo la Tagamenda katika barabara  kuu ya Iringa – Kilolo mmoja kati ya majeruhi alikimbizwa  Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili  na majeruhi   hao wengi  wao  walitibiwa na  kuondoka na hadi  sasa ni 20 ndio  ambao  wamebaki wakiwemo  wanaume 11  na wanawake 9 huku majeruhi  watatu  hali  zao ni mbaya na wapo katika uangalizi wa karibu  

 Jana  Kamanda  wa  polisi  wa  mkoa  wa Iringa Julius Mjengi  kati ya majeruhi hao yupo dereva  ambaye  pia ni mmiliki wa  basi la vitu  laini John  Upete (49) ambae  ameumia usoni na mguuni nahali yake inaendelea  vizuri

Wakati   dereva  wa  lori Fadhil Mbanga (25) yeye  alitoka   salama huku  mzee Lupyana Mtenga (70)  ambae  alikuwa amekaa siti ya  mbele akipoteza  maisha kwenye  ajali  hiyo .

Chanzo:Mtandao wa Godwin Francis
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment