Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, July 4, 2015

Urais CCM kumekucha, wanne waingia mitini na fomu

PAZIA la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kuomba kuteuliwa kuwania nafasi ya urais ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), limefungwa rasmi jana jion Kufungwa kwa pazia hilo kutoa nafasi sasa ya chama hicho tawala nchini kuingia katika hatua nyingine ngumu zaidi ya kufanya uteuzi wa nani anayefaa miongoni mwao kupeperusha bendera ya CCM. Tayari presha ya vikao hivyo vinavyotarajiwa kuanza wiki ijayo iko juu na baadhi ya wagombea na wapambe wao wako mjini hapa kwa ajili ya kufanya harakati za mwisho za kuomba kuteuliwa. Luhavi atangaza kufunga pazia Akitangaza kufunga pazia hilo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rajabu Ruhavi alisema kuwa zoezi hilo limefungwa rasmi jana huku wagombea wanne wakishindwa kurejesha fomu zao.. Alisema kuwa zoezi hilo lililoanza Juni tatu mwaka huu lilifanyika kwa utulivu na jumla ya wagombea 42 walichukuwa fomu na waliofanikiwa kurudisha fumu hizo ni wagombea 38 ambao walikamilisha masharti ya chama kwa kutafuta wadhamini katika mikoa 15 na kati ya hiyo, ikiwemo mikoa mitatu ya Zanzibar. Aidha Luhavi aliwataja walioshindwa kurudisha fomu ni Dk, Mussa Kolokola, Peter Nyalali, Helena Eliniwenga na Antony Chalamila. Hata hivyo Luhavi alisema mgombea mmoja aliyejulikana kwa jina la Helena Eliniwenga alizitelekeza fomu hizo katika moja ya ofisi za makao makuu ya chama siku aliyokuja kuchukua baada ya kulipia ada. “Eliniwinga baada ya kuchukuwa fomu aliingia katika moja ya ofisi za makao makuu ya chama na kuhitaji kupewa elimu ya siasa na utaratibu wa kupata wadhamini na alipoambiwa muda huo sio muafaka, alizitelekeza na kuondoka,” amesema Luhavi. Waliochukua na kurejesha fomu hizo ni Samuel Sitta, Dk. Ghalib Bilal, Dk. Asha Rose Migiro, Amos Siyantema, Malick Maruku, Agustino Mahiga, Makongoro Nyerere, Profesa Mark Mwandosya, Balozi Sefu Karume, John Magufuli, Boniface Ndengo, Mathias Chikawe, Titus Kamani, Steven Wasira, Sospeter Muhongo, Leonce Mulenda na Jaji Augustine Ramadhani. Wengine ni Benard Membe, Frederick Sumaye, Balozi Amina Salumu Ally, Mizengo Pinda, Harrison Mwakyembe, Mwele Malechela, Joseph Chaggama, Mwigulu Nchemba, Lazaro Nyalandu, Dk, Hamis Kigwangwala, Dk. Hassy Kitine, Luhaga Mpina, Eldfonce Bihole, Edward Lowassa, William Ngereja, January Makamba, Balozi Patrick Chokala, Mwalimu Banda Sonoko, Godwin Mwapongo na Rita Ngowi Chanzo:mwanahalisionline.com
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment