Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, March 13, 2015

Matokeo ya Mechi za ligi ya Europa

Mshambuliaji wa Everton, Romelu Lukaku jana aliisaidia timu yake ya Everton kupata ushindi dhidi ya Dynamo Kiev ya Ukraine wa magoli 2 kwa moja. Matokeo mengine ya mechi za mkondo wa kwanza wa ligi hiyo Villarreal ya Hispania ilishikishwa adabu na ndugu zao Sevilla baada ya kuchapwa jumla ya magoli 3 - 1. Zenit Saint Petersburg ya Urusi wakaiadhibu Torino ya italia kwa magoli 2 kwa 0. Nayo Fiorentina ya italia ikitoka sare ya goli moja kwa moja na AC Roma pia ya Italia. Napoli ya Italia wakawapa kipigo cha mbwa mwizi Dynamo Moscow ya Urusi cha magoli 3 kwa moja. Wolfsburg ya Ujerumani wakawa mwiba mkali kwa Inter Milan ya Italia pale ilipowashindilia magoli 3 kwa 1. Mechi za mkondo wa pili wa ligi ya Europa zitaendelea siku ya Alhamis ya wiki ijayo March 19 mwaka huu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment