Writen by
sadataley
3:55 PM
-
0
Comments
Wanajeshi wa Iraq na wapiganaji wanaopigana na wanamgambo wa Islamic State karibu na mji wa Tikrti wanasema kuwa kaburi na la rais wa zamani wa nchi hiyo Saddam Hussein karibu limeharibiwa kabisa.
Aidha zinaonesha picha za Saddam zikiwa zimeondolewa na mahala pake kuwekwa picha za viongozi wa wapiganaji ikiwemo picha ya jenerali wa Iran Qassem Soleimani anayewashauru wapiganaji wanaopigana vita na islamic state.
Mwaka uliopita jamii ya wasunni wanaokaa katika eneo hilo liliondoa mwili wa kiongozi huyo wa Iraq ambaye kungolewa kwake madarakani na majeshi ya muungano yaliongozwa na Marekani iliitumbukiza taifa katika vita ambavyo vimechacha hadi leo.
Haijulikani hadi wa leo ulizikwa wapi mwili huo.
Mwandishi wa BBC nchini Iraq anasema kuwa kuna shauku kuwa huenda wapiganaji wa Shia ndio walioharibu kaburi hilo ilikulipiza kisasi cha mateso waliyopita mikononi mwa kundi la Islamic state na wapiganaji wa Sunni.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments
Post a Comment