Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, March 10, 2015

DR MTITU ATANGAZA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KALENGA AMPONGEZA MBUNGE MGIMWA

MVUTANO mkali ubunge jimbo la Kalenga baada ya mpinzani wa Jackson Kiswaga kutoka kata ya Nzihi Msomi Dr Evaristo Mtitu kutangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Kalenga linaloongozwa na Godfrey Mgimwa (CCM) Akizungumza na wadau mbalimbali Dr. Evaristo Andreas Mtitu alisema kuwa amelazimika kujitokeza kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu mwaka huu kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema). Dr Mtitu alisema kuwa yeye ni mzaliwa Kidamali kata ya Nzihi katika halmashauri ya wilaya ya Iringa alizaliwa mwaka (1974) na kusoma Shule ya msingi Nyamihuu olevel Ulayasi secondary 1995. Alevel Mzumbe high school morogoro 1998, Pia baada ya hapo alijiunga na Stashahada ya ualimu Chuo cha ualimu Morogoro 2001. Shahada ya kwanza ya Elimu, Chuo kikuu DSM, 2006. Shahada ya uzamili katika elimu, Chuo Kikuu cha Charles Darwin, Australia, 2009. Dr Mtitu pia alisema amehitimu Shahada ya uzamivu (Doctor of Philosophy) katika elimu Chuo Kikuu cha VICTORIA cha Wellington, New Zealand, 2014. Akielezea kazi ambazo amepata kufanya katika nchi kuwa ni pamoja na ualimu Shule za sekondari , mkufunzi vyuo vya ualimu Tandala na Klerruu huku kwa sasa ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania aliyebobea katika taaluma ya mitaala ya elimu na ufundishaji, Katika Nyanja ya utandawazi alisema yeye ni mtafiti, elimu ya geography, sera mipango na uongozi katika elimu na nadharia ya upembuzi. Hivyo alisema kuwa lengo lake la kutaka ubunge jimbo la kalenga ni kushirikiana na wana Kalenga katika kuleta maendeleo . Kipaumbele chake ni kuboresha elimu na huduma za afya ,miundo mbinu huku akimpongeza mbunge wa sasa Bw Mgimwa kuwa amejitahidi kufanya kazi kulingana na uwezo wake kwa muda mfupi ila bado kuna haja ya kumuunga mkono kwa kumsaidia zaidi kwa kuliunganisha jimbo hilo na wahisani wa ndani na nje. Kujitokeza kwa Dr Mtitu katika kata hiyo ya Nzihi kutafanya kata moja hiyo kuwa na wagombea wagombea watatu hadi sasa wanaotaka ubunge kutoka kata hiyo .
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment