Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, February 24, 2015

IS yawateka wakristu 90 Syria

Kundi la Islamic State limewateka nyara watu 90 wa jamii ya wakristo kutoka katika kijiji kimoja kazkazini mwa Syria. Kisa hicho cha utekaji nyara kilifanyika mapema leo alfajiri, baada ya wanamgambo hao kuchukua udhibiti wa vijiji kadhaa kutoka kwa walinda usalama wa kabila la Wakurdi. Wanamgambo hao walivamia kituo cha Radio na kuchukua udhibiti wa mawasiliano na kuanza kutangaza Radioni, kuwa wamewateka nyara wale wanaojiita watetezi wa Dini. Kwa muda mrefu kundi la wakristo wachache walioko Nchini humo limekuwa likishirikiana na wapiganaji wa kabila la Wakurdi kukabiliana na wanamgambo wa IS. Awali Kundi la I S limekuwa likiharibu makanisa ya wakristo Nchini Syria. Wakristo hao wa makabila ya Assyria ambao wengi wamo serikalini, wanaiunga mkono utawala wa sasa wa Syria na wamekuwa wakipigana na wanamgambo hao wa Islamic State. Idadi ya Wakristo katika maeneo hayo imepungua kwa kasi mno kutokana na mauwaji dhidi yao.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment