Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 3, 2014

BRAZIL 2014: Walioongoza makundi wote waenda robo fainali


Wachezaji wa Colombia wakishangilia baada ya kufunga goli la pili dhidi ya Uruguay na kufuzu kuingia hatua ya robo fainali. 
Na Brasilia, BrazilBrasilia, Brazil. Historia mpya imeandikwa Brazil baada ya washindi wa makundi manane waliofuzu kucheza hatua ya 16 bora kuingia robo fainali.
Hiyo ni historia mpya tangu kuanza kwa Fainali za Kombe la Dunia 1930. Orodha hiyo ilikamilishwa juzi baada ya Ubelgiji kuilaza Marekani 2-1 kwenye muda wa ziada baada ya awali, Argentina kuiondoa Uswisi, pia kwenye muda wa ziada.
Mafanikio hayo ni mapya tangu kuanza kwa mfumo wa timu 32, hakuna mshangao kwa washindi hao kuingia hatua ya 16 bora.
Safari ya timu zilizofuzu kucheza robo fainali ambazo ni Brazil, Colombia, Uholanzi, Costa Rica, Ufaransa, Ujerumani, Argentina na Ubelgiji ilikuwa kama ifuatavyo:
Brazil
Ilimaliza mbele ya Mexico katika Kundi A ikiwa na pointi saba, ikailaza Chile 3-2 kwa penalti (baada ya sare ya 1-1) katika hatua ya 16 bora.
Wenyeji Brazil walikuwa na kibarua kuizima Mexico kwenye makundi vilevile mchezo dhidi ya Chile katika hatua ya 16 bora ulikuwa mgumu kwao, kiasi kwamba ilikuwa ni bahati kwao, Brazil kufuzu kwa penalti, pia mabao ambayo alifunga Neymar katika hatua ya makundi yaliibeba nchi hiyo.
Colombia
Walimaliza mbele ya Ugiriki katika Kundi C wakiwa na pointi tisa na wakailaza Uruguay 2-0 katika hatua ya 16 bora.
Kwa ujumla, Colombia ni timu ambayo imekuwa kivutio kikubwa katika fainali za mwaka huu. Waliongoza Kundi C kirahisi, kabla ya kuilaza Uruguay bila mtukutu Luis Suarez. Kibarua kigumu kwao ni kuwakabili wenyeji Brazil, kesho.
Uholanzi
Walimaliza mbele ya Chile katika Kundi B wakiwa na pointi tisa, wakaizima Mexico 2-1 katika hatua ya16 bora. Walianza vyema kwenye hatua ya makundi kwa kuwalaza waliokuwa mabingwa watetezi, Hispania kwa mabao 5-1 kabla ya kuwaondoa Australia.

Ushindi wao dhidi ya Chile ulikuwa wa kukamilisha ratiba kabla ya kuivaa Mexico katika mechi iliyokuwa ngumu. Katika mechi hiyo dhidi ya Mexico, mabao ya ‘jioni’ ya Uholanzi kutoka kwa Wesley Sneijder na Klaas-Jan Huntelaar yaliwapa tiketi ya kucheza robo fainali katika mechi iliyochezwa dakika 90.
Costa Rica
Walimaliza mbele ya Uruguay katika Kundi D, wakailaza Ugiriki 5-3 kwa penalti (baada ya sare ya 1-1) katika hatua ya 16 bora.
Ni sahihi kusema timu nyingine saba zilizobaki zina nafasi ya kutwaa taji hili, lakini Costa Rica wameduwaza wengi. Wamekuwa wakali mbele ya lango la mpinzani, wakifunga mabao na kuwaziba midogo wakali kama Italia na England.
Waliwatoa Ugiriki kwa penalti licha ya kucheza wakiwa 10 kwa dakika 60.
Ufaransa
Walimaliza mbele ya Uswisi katika Kundi E wakiwa na pointi saba na wakaiondoa Nigeria kwa mabao 2-0 katika hatua ya 16 bora.
Msimu huu, Ufaransa inamtumia vizuri mshambuliaji wake nyota, Karim Benzema akiwa katikati na wakati mwingine pembeni.
Katika mchezo dhidi ya Nigeria walionekana kupotea, lakini mabao ya dakika 11 za mwisho ya Paul Pogba na mlinzi Joseph Yobo aliyejufunga yaliwaokoa.
Ujerumani
Walimaliza mbele ya Marekani katika Kundi G wakiwa na pointi saba na wakaizima Algeria kwa mabao 2-1 kwenye hatua ya 16 bora.
Vita inayowasubiri kwenye Uwanja wa Maracana dhidi ya Ufaransa ni safari ambayo itatosha kuonyesha kuwa haikuwa ngekewa kuwatoa Algeria.

Walianza fainali hizi kwa makali kwa kuiadhiri Ureno. Katika mechi dhidi ya Algeria walionyesha udhaifu kwenye safu ya ulinzi, wakitegemea miujiza ya Thomas Muller akiwa kwenye kiwango.
Argentina
Walimaliza mbele ya Nigeria katika Kundi F wakiwa na pointi tisa na wakaiondoa Uswisi kwa mabao 1-0 katika hatua ya 16 bora.
Lionel Messi amekuwa ndiye mwokozi wao akiwa na mabao manne kibindoni.
Kwenye makundi walizilaza mapema Bosnia kwa mabao 5-1, Iran na Nigeria, lakini walitegemea miujiza ya Angel Di Maria kuitupa nje Uswisi katika hatua ya 16 bora.
Ubelgiji
Walimaliza wababe kwa Algeria katika H wakiwa na pointi tisa na wakaiondoa Marekani kwa mabao 2-1 kwenye muda wa nyongeza katika hatua ya 16 bora.
Hadi sasa wameshinda mechi zao zote, ingawa sifa yao imeingia doa kwa kukosa mfumo wa kuaminika wa kushambulia, kiasi cha kumaliza dakika 52 kwenye mechi zote bila hatari yoyote langoni mwa wapinzani. Juzi, walibadilika dhidi ya Marekani ambayo mikono ya kipa Tim Howard imemweka juu kwa kufanikiwa kuokoa michomo 15 ya hatari.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment