Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, June 24, 2014

YALIYOJIRI MAKANISANI TANZANIA KWA NJIA YA PICHA

Kama ilivyoada ya jumanne, GK inakupa fursa ya kutazama picha mbalimbali tulizokusanya kutoka makanisani nchini kujua yaliyojili katika ibada ya jumapili iliyopita katika makanisa hayo. Kwakuanza tunaanza na mkoani MWANZA ambako redio ya Kikristo ya HHC iliandaa tamasha la uimbaji lililofanyika katika viwanja vya kanisa la AIC Nyakato na kuhudhuriwa na waimbaji pamoja na waumini kutoka madhehebu mbalimbali.

Waimbaji wakimsifu Mungu.
Mmoja kati ya watangazaji wa radio ya HHC Maganga James mwenye shati nyeupe na tai akisikiliza uimbaji.
Lemi George akiwaongoza wenzake katika kumsifu Mungu.
Hakika ilikuwa safi sana kama inavyoonekana.
Mmmh shetani aliipata pata jumapili.
Waimbaji wakiwa wametulia wakicheza kwa madaha kumsifu Mungu. © Maganga James Gwensaga.
Baada ya kutoka Mwanza sasa ni jijini MBEYA ambako GK imefanikiwa kupata picha hizi za waumini wa kanisa katoliki mitaa ya jiji hilo wakiwa katika maandamano ya sherehe ya Ekaristi Takatifu ama Mwili na damu ya Yesu.
Gari likiwa limebeba bango la sherehe ya ekaristi takatifu.
Msafara wa ekaristi takatifu ukisonga mbele.
Watawa, waimbaji na waumini katika maandamano hayo.
Msafara wa Ekaristi kama unavyoonekana. ©Gershom Willy
Baada ya mkoani Mbeya na sasa ni huko mkoani KIGOMA ambako GK inapiga hodi hadi katika kanisa la Ufufuo na Uzima mkoani humo, ambao walikuwa na ibada nzuri ya matendo makuu ya Mungu kutendeka kama ilivyo kawaida ya jumapili zote, waumini walisikiliza neno pamoja na kuwa na kipindi cha kusifu na kuabudu bila kusahau 'Kupiga Majeshi'.

Mikono juu kuonyesha unyenyekevu kwa muumba wao.
Pia ibada hiyo ilikuwa na kipindi kizuri cha uimbaji.
Baadhi ya waumini wa kanisa la Ufufuo Kigoma wakiwa ibadani.
Jopo la watumishi wa kanisa la Ufufuo na Uzima Kigoma. ©Ufufuo Crew.

Baada ya mkoani Kigoma na sasa tunaelekea jijini Arusha ambako jumapili wapenzi wa muziki wa injili waliofika katika ukumbi wa hoteli ya Corridor Springs ya jijini humo walipata wasaa mzuri wa kushuhudia live recording iliyohusisha kwaya ya Tumaini Shangilieni pamoja na kwaya marafiki kutoka Mombasa Kenya ambao kwa pamoja kupitia sare zao nadhifu zenye kuonyesha bendera za nchi yao, walionekana wenye kupendeza na nadhifu haswa. Bila kusahau mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini Beatrice Muhone alikuwa sambamba kumtukuza Mungu na kwaya yake iliyomlea ya Tumaini.

Mambo yalikuwa mazuri kwakweli kama wanavyoonekana.
Wapigaji wa muziki wa kwaya ya Tumaini shangilieni wakiwajibika.
Tumaini na wageni wao wakiwa jukwaani.
Kwaya ya Upendo St. James wakimsifu Mungu.
Baadhi ya waimbaji wa Tumaini, mbele na kwaya ya Mombasa nyuma yao wakiwa wametulia katika ukumbi huo.
Angel akiwa na mwimbaji mwenzake wa Tumaini Beatrice Muhone wakiwa katika pozi la picha.
Baadhi ya wadada wa Shangilieni wakiwa katika pozi. ©Angel Minja & Samuel Kusamba.

Baada ya jijini Arusha sasa ni mkoani DAR ES SALAAM ambako tunaanzia huko mitaa ya Goba Matosa, katika kanisa la Tanzania Assemblies of God (T.A.G) City Light Temple kwa mchungaji Nimrodi Swai ambao licha ya ibada ya jumapili, walikuwa pia na mkutano wa Kiroho ambao ulifanyika baraka kwaa watu waliohudhuria.

Waumini wakiwa wamekaa kwa utulivu kusikiliza mkutano huo.
Kila mmoja alisimama au kukaa palipomfaa ili kusikiliza kilichokuwa kikiendelea.
Mtumishi wa Mungu akipaza sauti ya ukombozi.
Ilikuwa shangwe sana katika kumsifu Mungu. ©Sam Steven

Baada ya kutoka Goba, GK ikajisogeza mjini katika usharika wa Kilutheri Kijitonyama ambako kulikuwa na ibada kama kawaida, ambapo jumapili iliyopita walipata wageni Ukombozi kwaya kutoka Lutherani Msasani jijini Dar es salaam, ambao walifanyika baraka usharikani hapo kwa uimbaji wao.

Mrs Margaret Kato akiwaimbisha waimbaji wenzake wa Ukombozi Msasani.
Ukombozi Kwaya wakimsifu Mungu.
Kijitonyama Uinjilisti wakishambulia jukwaa.
Modest Morgan akiliongoza kundi la Kijitonyama Uinjilisti kumsifu Mungu. ©Onai Joseph
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment