Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, June 17, 2014

Viongozi wa dini walaani mauaji ya bomu Z’bar

Sheikh Ahmed Haidar Jabir akiwa amelazwa katika Hospitali ya Alrahma iliyopo Kilimani Zanzibar, baada ya kujeruhiwa na bomu na watu wasiojulikana na kusababisha kifo cha mtu mmoja. Picha na Mwinyi SadallahTanga. Kamati ya Amani na Uhusiano wa viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini Mkoa wa Tanga imelaani kitendo cha ulipuaji wa bomu mjini Unguja uliosababisha kifo cha mtu mmoja.
Akitoa taarifa ya pamoja na viongozi wa dini kulaani mauaji hayo, Sheikh wa Mkoa wa Tanga na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Juma Luwuchu aliitaka Serikali kuchukua hatua kuwasaka wote waliohusika na mlipuko huo.
Tayari Rais Jakaya Kikwete ameliagiza Jeshi la Polisi kuhakikisha linawatia mbaroni wote waliohusika na mashambulizi hayo yaliyosababisha maafa na kujeruhi wengine.
Alikemea tukio hilo na kuitaka jamii ya Watanzania kukataa matukio ya mauaji kama hayo kwa sababu yanahatarisha amani ambayo Watanzania wanajivunia.
Akifungua kikao cha kamati ya viongozi wa madhehebu ya Kiislamu na Kikristo Wilaya ya Tanga jana kuzungumzia mustakabali wa amani nchini, Sheikh Luwuchu alisema tukio la kuwaua viongozi wa dini kwa mabomu siyo kwamba limewashtua, bali pia limeleta taswira mbaya ya Tanzania kwa nchi nyingine duniani.
“Ili kukabiliana na matukio hayo ya mauaji, nimewaagiza viongozi wa madhehebu yote ya dini kupaza sauti zao kukemea kila wanapopata nafasi ya kuzungumza na waumini wao ikiwamo kulaani vitendo hivyo.
“Wanaoendesha vitendo hivyo wakiona kila kona wanalaaniwa wataona jamii haiwataki na hatimaye wataacha tu,” alisema Sheikh Luwuchu.
Pia alilaani mauaji ya albino, vikongwe na vitendo vya kumwagiwa tindikali vinavyoshamiri nchini akisema havina budi kupigwa vita kwa kushirikiana na Serikali.
Kabla ya kuanza kikao hicho, wajumbe wa kikao hicho ambao ni masheikh, maaskofu, wachungaji na mapadri walitembelea kituo cha vijana walioamua kuacha kutumia dawa za kulevya na kuzungumza nao juu ya masuala ya amani.
Wakiwa katika kituo hicho kilichopo Duga, wajumbe hao walielezwa na vijana hao juu ya changamoto wanazokabiliana nazo baada ya kuacha kutumia dawa za kulevya na kuomba jamii isiwatenge.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment