Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, June 16, 2014

UKWATA YAPATA RAIS WAKE MPYA, IRINGA MABINGWA MKUTANO TAIFA WAMALIZIKA

Mkutano mkuu wa taifa wa 49 wa umoja wa wanafunzi wa Kikristo Tanzania (UKWATA) umemalizika siku ya jana katika chuo cha ualimu Korogwe ikishuhudiwa umoja huo ukipata viongozi wapya pamoja na mkoa wa Iringa kuibuka mabingwa kwenye mashindano ya uimbaji.
 
Viongozi waliochaguliwa kushika hatamu ya mwaka 2014/2015 ni pamoja na Rais wa umoja huo bwana Laban Ndomkwa, makamu wake akiwa Vestina Sai, Katibu ni kijana Edward Kasawala, msaidizi wake ni mwanadada Neliwa Samweli huku mtunza fedha wa umoja huo akiwa Gerson Living. Pamoja na mengi yaliyotendeka ikiwa pamoja na vipindi vya maombi pamoja na neno ambavyo vimeshuhudia wanafunzi mbalimbali kufunguliwa na kusimamishwa upya ikiwa ni moja ya lengo la mkutano huo. 
 
Aidha pia katika suala la uimbaji mkoa wa Iringa umeibuka mabingwa kama ilivyotabiriwa kutokana na uimbaji wao wakichukua jumla ya maksi 156.5 za majaji wakifuatiwa na mkoa wa Dar es salaam na Pwani ambao huitwa DARPWANI waliochukua jumla ya maksi 156, namba tatu ilichukuliwa na wenyeji mkoa wa Tanga kwa jumla ya maksi 151 huku Ukwata kutoka makao makuu ya nchi mjini Dodoma wakiondoka na nafasi ya nne kwa maksi 145.5

 
Rais mpya wa Ukwata Tanzania Laban Ndomkwa.

Makamu wa Rais Ukwata Tanzania Vestina Sai

Katibu mkuu Ukwata Tanzania Edward Kasawala

Katibu msaidizi Neliwa Samweli

Mtunza fwedha Ukwata Tanzania Gerson Living.

Mambo ya uchaguzi yalivyokwenda.

Orodha ya viongozi wapya Ukwata Tanzania.

Wanaukwata wakipanda mabasi tayari kurejea makwao asubuhi ya leo.

Wakati kama huu huwa mbaya sana kwa wanafunzi wengi hasa baada ya kutengeneza marafiki kutoka kila kona ya nchi.

Safari salama mko na Yesu. shukrani kwa mwana GK na mdau wetu mkubwa Onai Joseph kwa matukio yote haya.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment