Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, June 17, 2014

Ujerumani 4-0 Ureno


Thomas Mueller ndiye mchezaji wa kwanza kufunga mabao matatu katika mechi moja Brazil
Thomas Muller alifunga mabao matatu na kuisaidia Ujerumani kuishinda Ureno mabao manne kwa nunge.
Mlinzi wa Ureno, Pepe alionyeshwa kadi nyekundu na kuondolewa katika mchuano huo.
Ujerumani, mabingwa mara tatu wa kombe la dunia, walionyesha mchezo wa kiwango cha juu.
Ujerumani ilichukua uongozi pale ambapo Thomas Muller alipopiga mkwaju wa penalti, baada ya Joao Pereira kuchezea vibaya Mario Goetze.
Mart Hummels alifunga bao la pili kupitia kichwa.
Pepe alionyeshwa kadi nyekundu muda mfupi baadaye kwa kosa la kumgonga Muller kwa kichwa.
Pepe alionesha kadi nyekundu baada ya kumgonga kichwa Mueller
Muller alifunga bao la tatu, ambalo lilikua lake la pili katika mchuano huo, kwa mkwaju wa kutoka karibu na lango.
Katika dakika ya 77, Thomas Muller aliongeza bao la nne la Ujerumani na kufanya idadi ya mabao yake katika mchuano huo kuwa matatu.
Muller anakuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao matatu katika mechi moja, kwenye kombe hili la dunia, mwaka 2014.
Kufuatia ushindi huu, Ujerumani inaongoza kundi hili kwa alama tatu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment