Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, June 14, 2014

Miezi miwili yatimia,matumaini hafifu ya kuwapata wasichana waliotekwa Chibok Nigeria

Wasichana waliyotekwa nyara na kundi la Boko Haramu, nchini Nigeria. Picha hii imepigwa kupitia mkanda wa video ambao umewekwa wazi na Boko Haram, Mei 12 mwaka 2104.
Wasichana waliyotekwa nyara na kundi la Boko 

Na Martha Saranga Amini
Raisi wa zamani wa Nigeria Olesegun Obasanjo ameonyesha hofu yake kuwa huenda wasichana waliotekwa na boko haram hawatapatikana wote wakati huu tukio la kutekwa kwa wasichana hao limetimiza miezi miwili hii leo tangu kutokea huku bado juhudi za kuwatafuta zikifanywa na wataalamu mbalimbali wa kimataifa wakilisaidia jeshi la Nigeria.

Akihojiwa na mtandao mmoja wa habari huko Nigeria bwana Obasanjo amesema kuwa hashawishiki kuamini kuwa wasichana hao wataweza kupatikana wote vinginevyo itakuwa miujiza.
Wapiganaji wa Boko Haram waliwateka wasichana wa shule takribani 276 katika shule moja katik akijiji cha Chibok, katika jimbo la kaskazini mashariki la Borno mnamo tarehe 14 mwezi wa nne.
Ni miezi miwili sasa, kuna dalili kidogo za wasichana Kuachiwa huru au kuokolewa, licha ya jeshi la Nigeria kusema kwamba walijua wapi wasichana walipofichwa baada ya kutekwa na jitihada za kimataifa kuendelea.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment