Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, June 17, 2014

Askofu ahofia uhai wa watoto

 
Dar es Salaam. Mauji ya watoto ni janga la dunia hivyo jamii inapaswa kuamka na kuchukua hatua kuikabili hali hiyo ambayo inapingana na mapenzi ya Mungu katika uumbaji wa binadamu.
Akizungumza kupitia Redio Maria, wakati wa kongamano la nne la kitaifa la Utoto Mtakatifu wa Yesu iliyofanyika katika Kanisa la Mt. Francisco Xvael, wilayani Tunduru Masasi jana, rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Tarcisius Ngalalekumtwa alisema mauaji ya watoto hivi sasa yanatisha.
Kongamano hilo ambalo lilifanyika ikiwa sehemu ya madhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika, Askofu Ngalalekumtwa alisema mauaji ya watoto kwa sasa yanapangwa na baba na mama.
“Wakati mwingine baba na mama wanaamua kuwa huyu mtoto hatumtaki, wanaamua kumnyonga, ni mauaji yanayotekelezwa na wazazi,” alisema maombi na sala zinahitajika kuikabili hali hiyo.
Hata hivyo, alionya kuwa mauaji hayo hayastahili kufanywa na jamii kwani kunyonga watoto ni kuondoa uhai wa Mwenyezi Mungu ambaye alimuumba kwa mfano wake.
Alisema ujumbe wa mwaka huu katika siku hiyo ni Kupata Elimu Bora Bila Vikwazo ni Haki ya Mtoto na kusisitiza kila mzazi anapaswa kutekeleza kwa vitendo.
Askofu Ngalalekumtwa alisema jamii ina jukumu la kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bora. Alitoa wito kwa viongozi wa kisiasa kudumisha amani nchini, Afrika na ulimwenguni.
Kuelekea maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika, kituo cha luninga cha TV 1 kimezindua shindano kwa vituo vinavyolea watoto na mshindi ataibuka na kitita cha Sh3.2 milioni.
Taarifa iliyotolewa jana, ilisema shindano hilo litaendeshwa kwa pamoja na wahisani wa Reach the Change ya Sweden, na litajulikana kwa jina la Game Changers.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment