Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 30, 2014

Mume atumai mkewe atanusurika kifo Sudan

Mume wa mwanamke aliyehukumiwa kifo kwa kuuasi uislamu na kuolewa na mkristo, ameielezea BBC juu ya matumaini yake kwamba rufaa yake itafaulu.
Dani Wani, mumewe Meriam Yahya Ibrahim, amemtembelea mkewe jela anakozuiliwa ambako amejifungua mtoto wa kike.
Dani Wani na wanawe, ameelezea matumaini yake kuwa rufaa ya mkewe itafaulu.
Amesema anahudumiwa vyema lakini mazingira hayo ya jela yamemuathiri sana mtoto wao wa kwanza.
Hukumu hiyo ya kifo kwa mwanamke huyo imeshtumiwa vikali na jamii ya kimataifa.
Ni matumaini yao kuwa rufaa hiyo itafaulu kabla ya mda wa miaka miwili aliyopewa kumwezesha kumnyonyesha mwanawe ipasavyo kukamilika.
Meriam alishtakiwa kwa kukataa kuurudia uislamu.
Nchini Sudan mwanamke wa kiislamu haruhusiwi kuolewa na mume asiyekuwa muislamu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment