Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, April 19, 2014

Bouteflika ashinda uchaguzi Algeria

Taarifa kutoka nchini Algeria zinasema kuwa Rais Abdelaziz Bouteflika ameshinda uchaguzi mkuu uliofanyika mnamo siku ya Alhamisi.
Bouteflika amekuwa akiugua Kiharusi kwa miaka mingi
Bouteflika alishinda uchaguzi huo kwa asilimia 80 ya kura na kupata nafasi ya kuongoza kwa muhula wa nne.
Hata kabla ya matokeo kutangazwa, kiongozi wa chama rasmi cha upinzani Ali Benflis, alisema kuwa uchaguzi huo ulikumbwa na wizi.
Bouteflika, ambaye amekuwa mamlakani kwa miaka 15, anakumbwa na hali mbaya ya kiafya kwani anaugua kiharusi na alipiga kura akiwa katika kiti cha magurudumu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment