Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, March 28, 2014

WORLD VISION YABADILI TAARIFA YAKE YA KUWAAJILI MASHOGA SIKU MBILI BAADA YA KUTANGAZA

Rais wa World Vision Richard Stearns.©Mtlmagazine
Shirika la Kikristo duniani la World Vision lenye makao makuu yake nchini Marekani limebadili uamuzi wake wa kuruhusu watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja kupata ajira ndani ya shirika hilo zikiwa ni siku mbili toka Rais wa shirika hilo Richard Stearns kutangaza kupitia taarifa yake siku ya jumatatu.

Baada ya Rais huyo kutangaza hatua ya shirika hilo taarifa ambayo imezua mkanganyiko miongoni mwa viongozi maarufu wa Kikristo ambao makanisa yao pamoja na taasisi hutoa misaada katika shirika hilo wakitaka makanisa na viongozi kususia uamuzi wa shirika hilo kwakuwa kwakuruhusu watu wanamna hiyo kufanya kazi ndani ya shirika hilo ni kwenda kinyume na neno la Mungu ambalo linapingana na vitendo vya mapenzi kwa watu wenye jinsia moja.

Katika taarifa mpya hapo jana Rais wa World Vision Richard Stearns hakuwa na jinsi zaidi ya kuomba msamaha kwa watu wote na viongozi wa makanisa mbalimbali ambao wamehuzunishwa ama kukwazwa na hatua iliyotaka kuchukuliwa na shirika hilo, na kutokana na mkanganyiko huo uliojitokeza shirika hilo limefuta kauli yake ya kutaka kuwaajili watu hao.

Lakini wakati Rais huyo akibadili uamuzi wa shirika hilo, tayari mwenyekiti wa makanisa ya Assemblies of God duniani George Wood amelitaka kanisa hilo pamoja na waumini wake ambao wamekuwa wakilisapoti shirika hilo, kuacha kufanya hivyo kwakuwa kanisa lao na mengine ya Kipentekoste yanafundisha kwakufuata Biblia.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment