Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, March 31, 2014

Musharraf ashitakiwa kwa uhaini Pakistan

Parvez Musharraf mtawala wa zamani wa kijeshi Pakistan
Mahakama moja nchini Pakistan imemsomea mashitaka ya uhaini mtawala wa zamani wa kijeshi Pervez Musharraf, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mkuu wa majeshi nchini humo kushitakiwa.
Bwana Musharraf anatuhumiwa kusitisha katiba kinyume cha sheria na kutangaza utawala wa sheria mwakai 2007.
Bwana Musharraf alikuwa rais wa Pakistan tangu mwaka 2001 hadi 2008, alikuwa mmoja wa watawala wa Pakistan waliokaa madarakani kwa muda mrefu.Amekana mashitaka na daima amedai kuwa mashitaka dhidi yake yana msukumo wa kisiasa. Atakabiliwa na adhabu ya kifo iwapo atapatikana na hatia.
Alikwenda kuishi uhamishoni mwaka 2008, na kurejea Pakistan mwezi Marchi 2013.
Alikuwa na matumaini ya kukiongoza chama chake katika uchaguzi, lakini alikosa sifa ya kugombea na kujikuta akikabiliwa na mashitaka yanayomhusisha na uvunjaji wa sheria akiwa madarakani.
Musharraf mwenye umri wa miaka 70 amekuwa hospitali tangu mwanzoni mwa mwaka huu na taarifa zinasema anatibiwa ugonjwa wa shinikizo la damu.
Wafuasi wa Bwana Musharraf wamefanya maandamano katika mji wa Karachi wakitaka hukumu ya haki itendeke. Jaji amemsomea Bwana Musharraf mashitaka matano.
Amekana mashitaka yote lakini pia aliiambia mahakama mchango wake kwa nchi ya Pakistan na kuhoji vipi aitwe msaliti, akisema yeye ni mzalendo.
"Naitwa msaliti, Nimekuwa mkuu wa majeshi kwa miaka tisa na nimelitumikia jeshi hili kwa miaka 45. Nimepigana vita viwili na huu ni 'usaliti'?" Shirika la Habari la Ufaransa, AFP, limemkariri askisema.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment