Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, February 28, 2014

Uhaba wa chakula. Sababu? Wewe

Uharibifu wa chakula
Ni kiasi gani cha chakula unachokitupa ambacho pengine ungekila?
Basi Ripoti mpya kutoka benki ya dunia inasema kuwa robo ya chakula chote kinachokuzwa duniani hupotea ama kutupwa, na sasa inawataka raia kufikiri kwa makini kile kuhusu uharibifu huu wa chakula.
Lakini katika jangwa la Sahara chakula kingi hupotea wakati wa uzalishaji.Inasema kuwa katika maeneo kama vile Marekani na Uchina ,watumiaji wa chakula ndio wa kulaumiwa pakubwa kwa kupoteza chakula hicho.
Benki ya dunia inasema kuwa kati ya asilimia 25 na 35 ya chakula chote kinachokuzwa duniani hutupwa.
katika mataifa yanye utajiri wa viwanda ,lawama kubwa zaidi huwaendea watumiaji wa chakula hicho ambao hukiwacha chakula kuoza katika jokovu.
Raia wa marekani kazkazini ni miongoni mwa wale walio na lawama kubwa kwa kuwa asilimia 61 ya chakula chao huharibika wakati wa matumizi.
Mwandishi wa ripoti hiyo Jose Cuesta anasema kuwa kile kinachohitajika ni kubadili tamaduni.
Lakini katika jangwa la Sahara chakula kingi huharibika wakati wa uzalishaji .
Benki kuu duniani inasema kuwa kiwango cha chakula kinachotupwa kinaweza kutofautisha kati ya chakula bora na uhaba wa chakula katika mataifa mengi.

Imeonya kuwa iwapo mbinu za uzalishaji hazitaimarishwa na tabia za kula kubadilishwa ,dunia huenda ikakumbwa na uhaba wa chakula kwa idadi kuu ya watu inayozidi kuongezeka.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment