Writen by
sadataley
11:00 PM
-
0
Comments
Msemaji wa Serikali ya Uganda, Ofwono Opondo, amewaambia waandishi wa habari mjini Kampala kuwa nchi yao haitishwi na mataifa ya magharibi kwa kukatisha misaada yao kwa sababu ya kukataa ushoga na kuongeza kuwa nchi yake itaendelea kujiendesha hata bila ya misaada yao.
Kauli ya Uganda inakuja kufuatia benki ya dunia kutangaza kusitisha msaada wa fedha kwa nchi ya Uganda uliokuwa unafikia kiasi cha dola milioni 90 kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya nchini humo.
Nchi za magharibi zimeendelea kutishia kusitisha misaada yao kwa nchi ya Uganda baada ya kupitishwa kwa sheria mpya ya kupiga marufuku wanaoendeleza mapenzi ya jinzia moja huku wadadisi wa maswala ya kiuchumi wakisema huenda nchi hiyo ikakumbwa na wakati mgumu.
Kauli ya Uganda inakuja kufuatia benki ya dunia kutangaza kusitisha msaada wa fedha kwa nchi ya Uganda uliokuwa unafikia kiasi cha dola milioni 90 kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya nchini humo.
Nchi za magharibi zimeendelea kutishia kusitisha misaada yao kwa nchi ya Uganda baada ya kupitishwa kwa sheria mpya ya kupiga marufuku wanaoendeleza mapenzi ya jinzia moja huku wadadisi wa maswala ya kiuchumi wakisema huenda nchi hiyo ikakumbwa na wakati mgumu.
No comments
Post a Comment