Writen by
sadataley
10:20 PM
-
0
Comments
Jeshi la Ufaransa limekua likilaumiwa na baadhi ya raia wa Jamuhuri ya Afrika ya kati hasa waislamu kwamba linaegemea upande wa wakristo, na kubaini kwamba jeshi hilo haliwajibiki vilivyo kwa kazi yake, hasa kufumbia macho vitendo vya mauwaji vinavyofanywa na kundi la vijana wa kikristo, Anti-balaka, dhidi ya waislamu.
Hata hivyo, Le Drian amesema kuwa ikiwa kutakuwa na haja ya kuongeza wanajeshi zaidi, hilo litafanyika baada ya wanajeshi wa Afrika chini ya kivuli cha Umoja wa Mataifa kupewa jukumu kamili la kuendeleza Operesheni ya kulinda amani mwezi ujao.
Mwishoni mwa mwezi wa desemba, rais wa kipindi cha mpito nchini Jamhuri ya Afrika ya kati Michel Djotodia pamoja na viongozi wa kidini waliwatolea wito wananchi wa taifa hilo wa kuachana na mauaji na badala yake kupendana na kuepusha tofauti zao za kidini na kuendelea kueshi kwa ushirikiano kama ilivyokuwa miaka ya hivi karibuni.
Wananchi wa Afrika ya Kati wanakabiliwa na ukosefu wa usalama na maelfu wamekimbia makwao, kipindi hiki majeshi ya Ufaransa na yale ya Umoja wa Afrika yakiendeleza Opereshenii ya kuyapokonya silaha makundi ya wapiganaji na kulinda amani.
Mapigano ya kidini nchini humo yamesabaisha maelfu ya watu kupoteza maisha.
Hata hivyo, Le Drian amesema kuwa ikiwa kutakuwa na haja ya kuongeza wanajeshi zaidi, hilo litafanyika baada ya wanajeshi wa Afrika chini ya kivuli cha Umoja wa Mataifa kupewa jukumu kamili la kuendeleza Operesheni ya kulinda amani mwezi ujao.
Mwishoni mwa mwezi wa desemba, rais wa kipindi cha mpito nchini Jamhuri ya Afrika ya kati Michel Djotodia pamoja na viongozi wa kidini waliwatolea wito wananchi wa taifa hilo wa kuachana na mauaji na badala yake kupendana na kuepusha tofauti zao za kidini na kuendelea kueshi kwa ushirikiano kama ilivyokuwa miaka ya hivi karibuni.
Wananchi wa Afrika ya Kati wanakabiliwa na ukosefu wa usalama na maelfu wamekimbia makwao, kipindi hiki majeshi ya Ufaransa na yale ya Umoja wa Afrika yakiendeleza Opereshenii ya kuyapokonya silaha makundi ya wapiganaji na kulinda amani.
Mapigano ya kidini nchini humo yamesabaisha maelfu ya watu kupoteza maisha.

No comments
Post a Comment