Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, January 27, 2014

Rais wa Ukraine awapa wapinzani nafasi za uongozi serikalini ili kutuliza ghasia za waandamanaji

Waandamanaji wanaopinga serikali ya Ukraine
Reuters/David Mdzinarishvili

Na Flora Martin Mwano
Wapinzani nchini Ukraine wameapa kuendelea na maandamano dhidi ya serikali ya Rais Viktor Yanukovych mpaka matakwa yao yatakapokamilika licha ya rais huyo kutoa nafasi za juu za uongozi kwa viongozi wa upinzani.

Jana jumamosi, Rais Yanukovych alitangaza kutoa nafasi ya Waziri Mkuu na Naibu Waziri Mkuu viongozi wakuu wa upinzani Arseniy Yatsenyuk and Vitali Klitschko ili kujaribu kutafuta suluhu ya machafuko hayo yaliyodumu kwa takribani miezi miwili.
Wakizungumza na maelfu ya waandamanaji mjini Kiev, viongozi hao wa wapinzani wamesema lengo lao sio tu nafasi za uongozi serikalini bali ni kutaka Taifa hilo lijiunge na ushirikiano wa kiuchumi na Umoja wa Ulaya EU.
Bado haijafahamika kama viongozi hao watakubali kushika nyadhifa hizo ama watazikataa na kuendeleza harakati zao.
Umoja wa Ulaya umeomba zichukuliwe hatua madhubuti kusitisha ghasia hizo, ambazo kwa mujibu wa wanaharakati tayari zimesababisha vifo vya watu watano na huenda hali ikawa mbaya zaidi endapo Rais Viktor Yanukovych ataamua kutumia nguvu zaidi kukabiliana na makundi ya waandamanaji walioingia mitaani takribani miezi miwili sasa.
Polisi wameendelea kukabiliana na waandamanaji katika mji mkuu wa nchi hiyo Kiev wakitumia risasi za mipira na
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment