Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, January 29, 2014

NJIWA WA AMANI WA PAPA FRANCIS WASHAMBULIWA MBELE YA UMATI

Purukushani na kusakwa kukiwa kumeanza, kunguru akifukuza wa kwake, shakwe akisaka wa kwake. ©AP
Katika hali isiyotarajiwa, ndege aina ya njiwa ambao walirushwa kutoka kwenye dirisha ambalo Papa Francis alikuwa akihubiria siku ya Jumapili kama ishara ya kutakia amani mataifa ya ulimengu ikiwemo Ukraine, ambayo iko kwenye machafuko kaw siku kadhaa sasa, walijikuta katika hali ya taharuki mara baada ya kushambuliwa na ndege wenzao aina ya kunguru na shakwe (seagull), makao makuu ya kanisa Katoliki Duniani, Vatican.

Njiwa hao ambao walipeperushwa na watoto waliokuwa sanjari na Papa kwenye kibaraza cha dirisha hilo, hawakupewa muda wa ziada, bali kuanza kushambuliwa kwa minajili ya kutumika kama kitoweo na ndege wenzao.

Hata hivyo katika shambulio hilo kwa njiwa hao ambao ni ishara ya amani, ambalo lilianza mara baada ya Papa na watoto hao kuondoka dirishani, njiwa mmoja alijiokoa kwa kuingia kwenye dirisha la ghorofa la chini yake, ilhali njiwa mwingine ambaye alikuwa akifukuzwa na kunguru, hatma yake haikujulikana mara moja mara baada ya kupoteza manyoya kadhaa mkiani alipokuwa akidonolewa na kunguru mara kwa mara.

Hapa watoto wakiwaachia njiwa wapae ©AP

Njiwa wakijipanga kwa safari. ©AP

Mpambano wa ndege ulipoanza, ndege aina ya shawe (seagull) akimshambulia njiwa wa 'amani' ©AP

Njiwa akiwa amedakwa mkiani na shakwe ©AP



Kunguru akifukuzia windo ©AP
Vurugu angani, njiwa kichwa chini mkia juu ©AP



kudonolewa kukiendelea ©AP


Picha zote kwa hisani ya Associated Press.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment