Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, January 4, 2014

Mazungumzo ya Sudan Kusini yakwama

Matumaini ya kupatikana kwa amani Sudan Kusini yameingia mashakani baada ya mazungumzo ya uso kwa uso ya pande zinazopingana yaliyokuwa yakitarajiwa kufanyika nchini Ethiopia kuchelewa.
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini
Waziri wa Mambo ya nje wa Ethiopia Tedros Adhanom amesema mazungumzo hayo yaliyokuwa yafanyike siku ya jumamosi hayatafanyika kama ilivyokuwa imetarajiwa.
Amesema mikutano inaendelea mjini Adis Ababa ili kuandaa agenda za mazungumzo hayo ya uso kwa uso ya pande zinazopingana.
Mwandishi wa BBC aliyepo Juba anasema mapigano makali yanaendelea. Ambapo pia majeshi yanayomuunga mkono rais Salva Kiir nayo yanajiandaa kwa mashambulizi katika eneo la Bentiu na Bor miji ambayo kwa sasa inashikiliwa na wafuasi wa Riek Machar aliyekuwa makamu wa rais wa zamani.
Amesema pande zote zinajaribu kuimarisha udhibiti wa kijeshi kabla ya kuanza kwa mazungumzo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment