Writen by
sadataley
6:40 PM
-
0
Comments
Msemaji wa rais wa taifa hilo Ye Htut amesema, rais Thein Sein ametekeleza ahadi yake kwa wananchi ya kwamba hakutokuwa na mfungwa wa kisiasa baada ya mwaka 2013. hata hivyo haikutajwa idadi ya wafungwa waliaoachwa huru kufuatia hatuwa hiyo ya msamaha wa rais na lini wataondoka jela.
Duru sahihi zimethibitisha kuwa takriban wafungwa tisa wa kisiasa wameachiwa huru hapo jana, miongoni mwao ni Yan Naing Tun aliye katika hukumu ya kifungo cha miezi minane kwa kutuhumiwa kushiriki katika maandamano ya amani jimboni Kachin lenye kukumbwa mara kadhaa na mashambulizi baina ya majeshi ya serikali na kundi la waasi kaskazini mwa Myanmar.
Yan Naing Tun aliwaambia waandishi wa habari kwamba anamuheshimu rais wa nchi hiyo baada ya kutekeleza ahadi yake.
Viongozi wa mashirika yanayo tetea haki za kibinadamu hususan Human Right Watch kupitia mmoja wa vingozi wake David Mathieson, amesema wameridhishwa na hatuwa hiyo na kusema kwamba ni ya muhimu.
Duru sahihi zimethibitisha kuwa takriban wafungwa tisa wa kisiasa wameachiwa huru hapo jana, miongoni mwao ni Yan Naing Tun aliye katika hukumu ya kifungo cha miezi minane kwa kutuhumiwa kushiriki katika maandamano ya amani jimboni Kachin lenye kukumbwa mara kadhaa na mashambulizi baina ya majeshi ya serikali na kundi la waasi kaskazini mwa Myanmar.
Yan Naing Tun aliwaambia waandishi wa habari kwamba anamuheshimu rais wa nchi hiyo baada ya kutekeleza ahadi yake.
Viongozi wa mashirika yanayo tetea haki za kibinadamu hususan Human Right Watch kupitia mmoja wa vingozi wake David Mathieson, amesema wameridhishwa na hatuwa hiyo na kusema kwamba ni ya muhimu.
No comments
Post a Comment