Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, January 2, 2014

Kamanda wa DRC auawa vitani Kivu

Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Lambert Mende, amesema kuwa kamanda wa majeshi ya serikali yanayopigana dhidi ya kundi la wapiganaji wa kiisilamu wa Uganda, mashariki mwa nchi ameuawa.
Kamanda Ndala aliuawa baada ya kuviziwa na waasi wa ADF-Nalu
Kanali Mamadou Ndala alifariki baada ya kuviziwa na waasi katika mkoa wa Kivu Kaskazini.
Waasi wa ADF-Nalu ndio waliofanya shambulizi hilo.
Kanali Ndala alihusika katika juhudi za kijeshi dhidi ya kundi la waasi wa M23 mwezi Novemba mwaka jana na hasa aliongoza kikosi cha jeshi dhidi ya waasi hao wa ADF-Nalu.
Jeshi la Congo, likiungwa mkono na wanajeshi wa Umoja wa mataifa linapambana na makundi ya waasi waliojihami Mashariki mwa nchi.
Eneo hilo linapakana na Uganda, Rwanda na Burundi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment