Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, January 29, 2014

Jaribio la kumuua waziri Libya latibuka

Kumekuwa na jaribio lililotibuka la kumuua kaimu waziri wa ndani nchini Libya Al-Sidik Abdel-Karim.
Libya imekuwa ikikumbwa na msukosuko wa kisiasa tangu Muamar Gadaffi kuuawa
Shirika la kitaifa la habari LANA na lile la AFP yamethibitisha tukio. Inaarifiwa kwamba gari alimokuwa Abdel Karim lilipigwa risasi alipokuwa akielekea katika mkutano katika makao makuu ya bunge.
Abdel-Karim anatarajiwa kuhutubia waandishi habari hivi punde.
Abdel Karim aliteuliwa na waziri mkuu nchini Libya kuwa kaimu waziri wa ndani baada ya waziri Mohamed Sheikh kujiuzulu mnamo Agosti mwaka jana.
Seddik Abdelkarim, alikuwa katika gari lake aliposhambuliwa na watu wasiojulikana waliomfyatulia risasi. Inaarifiwa hakuna aliyeuawa kwenye shambulizi hilo.
Libya imekuwa ikikabiliwa na hali ngumu ya kisiasa tangu waasi kuipindua serikali na kumuua aliyekuwa Rais Muamer Kadhafi mwaka 2011.
Waziri huyo alikuwa njiani kuelekea bungeni wakati gari lake liliposhambuliwa.
Shambulizi lenyewe limetokea chini ya wiki tatu baada ya mauaji ya naibu waziri wa viwanda Hassan al-Droui, aliyeuawa mjini Sirte
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment