Writen by
sadataley
1:40 PM
-
0
Comments
Hatimaye Iran na mataifa sita yenye nguvu duniani wamefikia makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran, Kiongozi Mkuu wa mjadala huo Bi, Catherine Ashton amethibitisha hilo baada ya takribani siku tano za majadiliano makali ya mjini Geneva nchini Uswisi. Mataifa yenye nguvu duniani ambayo ni Uingereza, Marekani, Urusi, China, Ufaransa na Ujerumani wamekuwa na madai ya kutaka Tehran isitishe urutubishaji wa uranium ili iondolewe vikwazo inavyokabiliwa navyo.
No comments
Post a Comment