Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, October 6, 2013

Makundi ya wapiganaji Kaskazini mwa Mali yahimizwa kurejea katika mazungumzo ya amani na serikali ya Bamako

Wapiganaji wa Tuareg Kaskazini mwa Mali
Na Flora Martin Mwano

Balozi wa Umoja wa Mataifa UN nchini Mali, Bert Koenders amehimiza kundi la wapiganaji la Tuareg na waasi wa kiarabu kurejea katika mazungumzo ya amani na serikali ya Mali ili kuhitimisha mzozo unaondelea kutatiza usalama wa Kaskazini mwa nchi hiyo.
Katika mazungumzo yake na Rais wa Burkina Faso Blaise Compaore, Koenders ametoa mfano wa mapigano yaliyoshuhudiwa hivi karibuni na kuyasihi makundi hayo kushiriki katika mazungumzo na serikali ya Bamako ili kurejesha usalama wa Taifa hilo la Magharibi mwa Afrika.
Mwishoni mwa mwezi Septemba, waasi hao walitangaza kujitoa kwenye mazungumzo ya amani yaliyokuwa yakiendelea kati yao na serikali ya Rais mpya wa nchi hiyo Ibrahim Boubacar Keita.
Mwishoni mwa mwezi Septemba, waasi hao walitangaza kujitoa kwenye mazungumzo ya amani yaliyokuwa yakiendelea kati yao na serikali ya Rais mpya wa nchi hiyo Ibrahim Boubacar Keita.
Siku moja baada ya uamuzi huo kutolewa mapigano mapya yalizuka eneo la Kaskazini mjini Kidal ambapo wanajeshi wawili wa serikali walijeruhiwa katika shambulio la guruneti.
Kwa mujibu wa serikali ya Bamako, shambulio hilo lilifuatiwa na na jingine mjini Timbuktu ambapo wananchi wawili waliuawa na wanajeshi sita kujeruhiwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment