Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, September 5, 2013

Mkutano wa G20 waanza Syria ikitokota

Viongozi wa mataifa wanachama wa kundi la G20 wanakusanyika katika mji wa St Petersburg nchini Urusi kwa mkutano wao wa kila mwaka wa mataifa ishirini yenye ustawi mkubwa wa kiviwanda duniani.
Urusi ndio mwenyeji wa mkutano wa G20
Duru zinasema maswala ya kiuchumi huenda yakafumbiwa macho katika mkutano huo kutokana na mzozo uliopo nchini Syria na tofauti zilizopo kati ya Marekani na Urusi kuhusu mipango ya kuishambulia Syria kwa madai ya kutumia silaha za kemikali.

Naye Rais Vladimir Putin amesema kuwa Marekani ikishambulia Syria litakuwa tendo la uchokozi. Rais wa Marekani ameeleza kwamba Serikali ya Syria imekaidi marufuku ya kimataifa ya kutumia silaha za kemikali na hatua inapaswa kuchukuliwa.Rais Barack Obama anasema kuwa dunia haiwezi kuepuka tendo la kutochukua hatua dhidi ya Serikali ya Syria.
Kiongozi wa Urusi anasema vingine kuwa Marekani kushambulia Syria bila idhini ya Umoja wa Mataifa ni kukiuka sheria ya kimataifa.
Hapa hali ya maoni mawili yanayohitiliafiana kutoka kwa Marais wawili maarufu.
Inaonekana kuwa tofauti kubwa inayohusu Syria huenda ikapata nafasi bora katika vyombo vya habari kuliko mkutano unaoendelea wa mataifa tajiri zaidi duniani ya G20. Marais hawa wawili ni wanachama wa G20 ambapo watataka kushawishi mataifa kuunga mkono upande wao.

« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment