Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, September 4, 2013

Diwani wa CCM atishia kujiuzulu nafasi yake

Na Ahmed Makongo
Bunda. Diwani wa Kata ya Kisorya wilayani hapa, Misana Jigwira (CCM), amesema yuko tayari kuachia nafasi yake kwa kujiuzulu, iwapo mganga mkuu mfawidhi wa kituo cha afya cha kata hiyo hatahamishwa kazi.
Jigwira alisema atachukua hatua hiyo kutokana na mganga huyo, kutokuwajibika ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kutokuwapatia dawa wagonjwa wanaofika kituoni hapo licha ya kuchangia fedha papo kwa papo kiasi cha Sh1,000 kwa kila mgonjwa na kwamba kwa sasa fedha hizo zimeongezeka na kufikia Sh3,000.
Diwani huyo bila kutafuna maneno alisema licha ya wagonjwa hao kuchangia fedha hizo, huambiwa na mganga huyo kwamba dawa hazipo na kuwaagiza waende kununua kwenye maduka ya watu binafsi.
Alisema kutokana na kero hiyo wananchi wamekuwa wakifika kwake mara kwa mara kulalamikia hali hiyo, ikiwa ni pamoja na huduma duni wanazopata kwenye kituo hicho.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment