Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, September 10, 2013

Bensouda:'Ruto alimiliki jeshi la kivita'

Naibu rais wa Kenya William Ruto amekana mashitaka ya uhalifu katika kesi inayoendeshwa kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC , Hague Uholanzi.
Bwana Ruto na wafuasi wake alipokuwa anaondoka Kenya kuelekea Hague
Bwana Ruto -- ambaye anatuhumiwa kupanga ghasia za baada ya uchaguzi uliokuwa na utata wa mwaka 2007 -- amekana mashtaka hayo sawa na mshitakiwa mwenza katika kesi hiyo mtangazaji Joshua Arap Sang.
Mwendesha mkuu wa mashtaka katika ICC, Fatou Bensouda, alimtaja Ruto kuwa mwanasiasa shupavu ambaye alipanga kufanya uhalifu dhidi ya binadamu ili kujinufaisha kisiasa.
Amesema kuwa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007, Ruto aliunda jeshi lake la kivita kumpigania dhidi ya mahasimu wake madai ambayo yamekanushwa na wakili wa Ruto bwana Khan
Bwana Ruto na Rais Uhuru Kenyatta pamoja na mwandishi wa habari Joshua Arap Sang, wanatuhumiwa kwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007, kufanya mauaji kuchochea na kupanga ghasia hizo.
Rais Uhuru Kenyatta ambaye pia anatuhumiwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu, anatarajiwa kufikia katika mahakama hiyo mwezi Novemba
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment