Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, August 14, 2013

JAJI AAMURU MTOTO KUTOITWA MESSIAH, 'MESSIAH NI YESU TU' ASEMA.


Mtoto akiwa bize na mama yake (picha hii haina uhusiano na mtoto aliyeandikwa kwenye habari.) ©Dreamstime 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Jaji moja Tennessee ameamuru mtoto kubadilishwa jina kutoka kuitwa Messiah na kwenda Martin, akisema kuwa jina hilo sio zuri kwenye mazingira ya mtoto huyo kukulia.
Jaji Lu Ann Ballew ambaye amesema kuwa mtoto huyo atapata shida kutoka kwenye jamii ya watu wa eneo analoishi na kwamba mtoto huenda asingekubali kutokana na shida ambazo atapata mtaani kutokana na kuchaguliwa jina, amepingwa na mama mzazi wa mtoto huyo mwenye umri wa miezi 7, ambaye amepewa jina la Messiah DeShaw Martin.
"Messiah ni cheo, na kimepatikana kwa mtu mmoja tu, na huyo mtu ni Yesu Kristo." Jaji Ballew alikiambia kituo cha habari cha WBIR.
Chanzo cha dhahama hiyo kama ambavyo inaonekana kwa mama wa mtoto huyo, ni pale ambapo wazazi (yeye na mumewe) walishindwa kukubaliana kuhusu jina la mwisho la kumpa mtoto, na hatimaye kwenda kwenye mahakama ya malezi ya mtoto ambapo Jaji akaja na uamuzi wake.
Hata hivyo mama wa mtoto huyo amesema kuwa atakata rufaa kutokana na maamuzi ya jaji huyo, kwani hayajamridhisha hata kidogo na kwamba hakuyategemea.
Chanzo: Blog ya Gospel kitaa
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment