Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, August 15, 2013

Idadi ya vifo Misri yazidi kuongezeka

Mwandishi wetu anasema aliona miili 140 ikiwa imefungwa kwenye sanda.
Wengi wa waathiriwa walifariki dunia katika mji mkuu wa Cairo lakini kulikuwa na vurugu katika maeneo yote ya nchi katika siku iliyoshuhudia umwagikaji mkubwa wa damu tangu mapinduzi ya kidemokrasia yaliyotokea miaka miwili iliyopita.
Idadi kamili inaaminika kuwa juu zaidi kwa kuwa miili mingi ya waliofariki dunia bado haijasajiliwa.
Wafuasi wa rais Mohammed Morsi, aliyeng'olewa marakani mwezi uliopita wanasema zaidi ya watu 2,000 waliuwawa.
Mwandishi wa BBC Khaled Ezzelarab ameripoti kuwa ameshuhudia zaidi ya miili 140 ikiwa imefungwa kwenye sanda katika Msikiti wa Eman, uliopo karibu na kambi ya maandamano ya Rabaa al-Adawiya.
Vugugu la Undugu wa Kiislamu, Muslim Brotherhood, ambalo linamuunga mkono bwana Morsi, linapanga maandamano mengine mjini Cairo na mji wa pili kwa ukubwa, Alexandria, kulalamikia mauaji hayo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment