Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, August 16, 2013

ASKOFU DR. OWDENBURG MOSES MDEGELLA: KATIBA IJALI HAKI NDIPO UTU UTAKUWEPO,SERIKALI YA TATU NI ULAJI TU NA NI AIBU KWA BARA LA AFRIKA

 
       Baba Askofu Dkt. Owdenburg Moses Mdegella akizungumza na Waandidshi wa Habari
   Hapa alipokuwa akitoa ufafanuzi wa muundo na namna aonavyo Serikali zinavyoweza           shirikianaWaandidshi wa Habari
Baaadhi ya Waandidshi wa Habari
Hayo ameyasema leo hii alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa Mkoa wa Iringa. Baba Askofu alikuwa akizungumza juu ya Katiba na Muungano. Alitoa makzo kuwa viongozi wetu wote wamejilimbikizia mali hivyo tofauti kati ya masikini na matajiri ni kubwa sana. 

Akizungumzia juu ya Uraia wa Muungano alikubaliana nao kwani unatokana na kuzaliwa mahali husika. Kumbe vitambulisho vyetu vya uraia vitaandikwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hapa sasa  tunazungumzia raia wa nchi moja na si vinginevyo. Hebu tutazame maoni ya wanaotaka serikali moja, mbili na tatu na kisha walete yale maoni kwa maana ya mtazamo wetu wa kimaongozi kama ni serikali tatu,mbili au moja.

Hivi kweli kuna ndoa inayoruhusu kugawana vyumba, huo ni udanganyifu. Hivyo sura ya 6-7 za rasimu ya katiba hadi aya ya 84 hivi zinapaswa kubadilika.
Tunapaswa kuwa na serikali mbili aua moja tu , tuzingatie hali ya wananchi wa kawaida na si uchama au ushabiki fulani. Hivi hii serikali ya tatu itatawala vipi na makao yake yatakuwa wapi?Hivi kweli mtu wa kawaida wa kijijini anataka serikali tatu yeye anataka apate soko la mazao yake tu.

1Samweli 8:4-18(OMBI LA KUPEWA MFALME)-Hapa wamemkataa Nyerer na Karume na wanawagombanisha wakati wamekufa.Ni nai asiyejua msimamo na mwelekeo wa Mwl. Nyerer?
Wapo wanasiasa  wenye matamanio yao (Self personal Interest)ambao wanataka madaraka. Kiongozi anatangaza vita ila yeye na mkewe wamejifungia ndani. Hivyo wa kuumia ni Wananchi tu.

Marais  watakao watawala watawatawala ninyi na watoto wenu, hebu tutazame maslahi ya taifa na si chama na tusishabikie mambo tusiyoyajua. Hebu tuunde Tume (Commision) sote tuwe na Katiba huru zitakazo tuongoza, sivyo wagawane muda wa maongozi yaani miaka miwili na nusu. Waongoze kwa zamu na uwe Muungano katika serikali mbili na si tatu.

Tuwe na mambo ya pamoja
1.Udugu sote tunahitajiana na soe tunandugu pande zote.
2.  Jeshi ni lazima tuangalie yanayotokea  Somalia, Nigeria na Kongo hivyo tunapaswa kuwa makini sana,
3. Sarafu moja
4. Ardhi
5. Bunge la Muungano
.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment