Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, July 8, 2013

YESU ANATUITA TUWE WAMISIONARI

"Yesu anatuita tuwe Wamisionari ni sisi sote  tulioitwa kwa nafasi zetu , waamini wote na wale wanaotenda mema  kwa wengine".

Papa Francis akizungumza na waamini pembeni amezungukwa na viongozi waandamizi wa Vatican.
Hayo yamesemwa na Papa Ffrancis alipokuwa akizungumza na waamini katika uwanja wa Mtakatifu Petro huko Vatikan.Baba Mtakatifu amesema sote(tunaoamini)tunaitwa na tunaalikwa kuwa Wamisionari kwa wengine kwani Yesu alipokuwa akiwatuma wale sabini na wawili(72)si kwamba sisi alitutenga hapana nasi tumealikwa kwa utume huo.

Papa francis amesema kuwa kwa upendo na wema wa  Bwana wetu Yesu Kristo alitualika nasi tulioamini baada ya Mitume kwamba nasi tunapaswa  kuwafanya wengine wamuone Mungu kupitia sisi. Hivyo basi kwakufanywa kuwa wafuasi (discipleship) tunapaswa kuonyesha ukuu na wema wa Mungu kwa wengine.Tunaposema kuonesha ukuu na wema wsa Mungu si kwa kuaa nao au kupoteza muda la  bali ni kuwatangazia ukuu wa Ufalme wa Mungu.

Akifafanua zaidi Baba Mtakatifu amesema wale Mitume kumi na wawili (12 Disciples) wanawakilisha Maaskofu na wale sabini na wawaili (72) wanawakilisha watumishi wengine katika Kanisa na waamini wote ikiwa ni pamoja na wale wanaotenda matendo yote ya huruma.
Na siku zote nguvu za Mungu zi pamoja nasi  "Shetani hana nguvu mbele ya Mungu"
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment