Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, July 8, 2013

Papa Francis awakumbuka wahamiaji Italia

Papa Francis amesherekea maisha ya mamia ya wahamiaji wa kiafrika waliokufa maji wakijaribu kufika baya Ulaya. Akiwa ziarani katika kisiwa cha Lampedusa Papa aliabiri mtumbwi mdogo na kuweka shada la maua ndani ya bahari ya shamu. Kisha alifanya dua ya pakee. Baadaye amekutana na baadhi ya wahamiaji.
Papa Francis amewakumbuka mamia ya wahamiaji wanaokufa maji wakitaufa maisha 
Pope Francis meets a group of immigrants at the pier in Lampedusa, Italy
Papa akisaliamiana na baadhi ya Wahamiaji huko  Lampedusa
Ziara hii ya papa nje ya mji wa Vatican haina mbwembwe, aliwasili kisiwa kidogo ambacho kimekua makao ya maelfu ya wahamiaji haramu wa Kiafrika na kisha baadaye kutumia mtumbwi kuelekea baharini.
Akiwa kwenye bahari ya shamu Papa ameweka shada la maua ya njano kama ishara ya kuwakumbua maelfu ya wahamiaji haramu ambao wamekufa maji wakijaribu kufika kisiwa hicho, kinachotumiwa kama kivukio kwenda barani Ulaya.
Katika bandari ya kisiwa hicho papa amesherekea ibada maalum na baadhi ya wahamiaji na kisha baadaye kurejea makao makuu ya Vatican.
Papa Francis ni mwanawe mhamiaji kutoka Italia ambao waliishi nchini Argentina. Akiwa Askofu mkuu wa Buenes Aires alilaani unyanyasaji wa wahamiaji na kufananisha dhuluma hizo kama utumwa.
habari kwa hisani ya bbc swahili
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment