Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 19, 2013

Watumiaji wa Intaneti nchini wafikia mil 5.9

Na Brandy Nelson
 Mbeya. Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu milioni 5.9 Juni mwaka jana, ilielezwa.
Ofisa wa Idara ya Maendeleo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) wa TCRA, Connie Francis aliyasema hayo wakati wa semina ya wadau wa mtandao wa Intaneti iliyohusisha uundaji wa kamati ya mpito ya uanzishwaji wa Kituo cha ‘Mbeya Internet Exchange Point’.
Alisema kutokana na umuhimu wa huduma ya intaneti kwa shughuli mbalimbali, idadi ya watumiaji wa huduma hiyo nchini imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu milioni 5.9 mwaka jana.
Alisema huduma hiyo imerahisisha utoaji wa huduma mbalimbali za kibiashara, kiuchumi na kijamii.
Francis alisema kuwa baada ya kuonekana umuhimu wa huduma hiyo TCRA imeamua kuanzisha mradi ambao utamsaidia mtumiaji kupata huduma hiyo kwa ubora, urahisi na haraka zaidi na kwa gharama nafuu.
Alisema katika kituo hicho watoa huduma wataweza kuweka vifaa vyao na kupata fursa ya kuungana na kurahisisha maendeleo ya mtandao wa Intaneti na kwamba itaisaidia nchi kudhibiti mawasiliano ya ndani na kubaki ndani ya nchi badala ya kutoka nje ya nchi na kurudi ndani.
“Mfumo uliopo kwa sasa ni pale mtumiaji wa mtandao wa Intaneti mawasiliano yake kwenda nje ya nchi ya Tanzania na kurudi hapa kwetu na ndipo baadae kuja kumfikia mhusika. Ni mfumo unaochukua muda mrefu na gharama kubwa kutokana na mzunguko uliopo’’ alisema.
Tayari kamati ya mpito ya uanzishwaji wa kituo hicho imeundwa ambapo imeshirikisha wadau wa mtandao wa Intaneti na itakabidhiwa ofisi pamoja na vifaa hivyo kwa ajili ya kuanza kazi .
ya kusimamia mfumo huo mpya na kuhamasisha watoa huduma ya mtandao wa Intaneti kujiunga na kituo hicho kwa ajili ya kufanya kazi kwa ufanisi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment