Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 24, 2013

Njama ya uasi yatibuka Ivory Coast

Njama ya uasi pamoja na jaribio la wafungwa kutoroka jela kubwa zaidi nchini Ivory Coast imetibuka na kusababisha vifo vya wafungwa wawili.
                           Gereza la Maca ambako wahalifu sugu wanafungwa
Polisi walilazimika kurusha gesi ya kutoa machozi pamoja na kufyatua risasi ili kutuliza hali katika gereza la Maca mjini Abidjan.
Maafisa wanasema kuwa walinzi wawili wa magereza walijeruhiwa vibaya.
Purukushani lilizuka Jumanne jioni wakati wafungwa kadhaa walipovunja milango ya magereza yao na kuwaachilia huru baadhi ya wafungwa.
Gereza hilo huwahifadhi wahalifu sugu na baadhi ya maafisa kutoka kwa iliyokuwa serikali ya rais wa zamani Laurent Gbagbo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment