Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 18, 2013

K.K.K.T DAYOSISI YA IRINGA KUWASAIDIA WAJANE, YATIMA NA WAGANE, NI KUPITIA MRADI WA MBUZI

MRADI HUO UNATARAJIA KUANZA MAPEMA MWEZI UJAO  NA UTAWANUFAISHA ZAIDI YA WATU 170 KWA AWAMU YA KWANZA.
MRADI HUO UNATARAJIWA KUTEKELEZWA KATIKA SHARIKA  ZA KILOLO NA KILENGA PASI (LUGANGA).
   MCHUNGAJI YONA  KINGANGA 
MCHUNGAJI KIONGOZI USHARIKA WA KILOLO

Hayo yamesemwa na Mchungaji Yona Kinganga pichani akisema kuwa mradi huo wa mbuzi unatarajiwa kuanza mapema mwezi ujao. Akiendelea kutoa maelezo amesema  kuwa jumla ya mbuzi 175 zitagawiwa  huku  majike  yakiwa ni mia moja sabini (170) na madume  matano (5). Walengwa watakao nufaika na mradi huo ni wajane, yatima na wagane  toka katika sharika mbili Usharika wa Kilolo na Usharika Mpya wa Kilengapasi(Luganga) ambao kwa kweli Kanisa limeridhia na kuona wanahitaji kupewa nafasi ya kuingizwa katika mradi  huo. 
Mchungaji Kinganga alitoa mkazo kuwa ni watu mia moja sabini watakaoanza na ni  wale  wasio na uwezo kabisa huku wakiwa na wajibu wa kusomesha watoto. 
Mradi huu ni sehemu ya matunda ya mahusiano ya Usharika wa Kilolo na Swideni na kwamba siku ya Jumamosi hii( 20/07/2013) itafanyika semina elekezi katika usharika huo ambapo wawezeshaji ni shirika la Navigator toka Morogoro.
Na pia akasema kuwa maandalizi ya mabanda ya kufugia yamekwisha anza na tayari walishapewa ramani  inayoelekeza namna ya kujenga. 
               Mfano wa banda la kufugia mbuzi likiwa katika hatua za mwisho kukamilika
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment