Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, March 2, 2018

Hali ya kawaida yarejea katika Ubalozi wa Ufaransa jijini Ouagadougou

Hali imerejea kama kawaida katika Ubalozi wa Ufaransa jijini Ouagadougou nchini Burkina Faso baada ya wavamizi wanne waliokuwa wamekwenda kuvamia Ubalozi huo wa nchi hiyo, kituo cha utamaduni na makao makuu ya jeshi nchini humo.
Serikali ya Burkina Faso imethibitisha kuuawa kwa wavamizi hao ambao kwa mujibu wa watu walioshuhudia, watu watano waliokuwa wamejihami kwa silaha walishuka ndani ya gari na kujaribu kushambulia Ubalozi huo.
Waziri wa Mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesema hakuna raia yeyote wa Ufaransa aliyejeruhiwa katika tukio hilo na taasisi zote za serikali ya Ufaransa zipo salama.
Baada ya shambulizi hili, Ubalozi wa Ufaransa nchini humo umewaambia raia wake kusalia nyumbani huku rais Emmanuel Macron akisema amekuwa akifahamishwa yale yote yaliyokuwa yanafanyika.
Shambulizi hili limekuja wakati huu Ufaransa ikiwa katika mstari wa mbele kuyasaidia mataifa katika ukanda wa Sahel ikiwemo Burkina Faso kupambana na makundi ya kjihadi.
Ufarans imetuma wanajeshi wake 4,000 katika mataifa hayo ambayo pia yanaundwa na Chad, Mali, Mauritania na Niger.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment