Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, March 17, 2018

FITINA ZA WAARABU ZAANZA, MSAFARA WA SIMBA WAPIGWA STOP KUELEKEA UWANJANI


Msafara wa Simba SC kuelekea Uwanjani Port Said, umezuiliwa na viongozi wa soka nchini humo.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni saa moja tu limesalia kuelea mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Al Masry dhidi ya Simba.

Simba wamelazimishwa kupanda basi tofauti na lile walilokuwa wamepangiwa awali, hivyo kusababisha kuleta mzozo.

Aidha, uongozi wa Simba umeshtukia mchezo mchafu wa Waarabu, pengine kunawezekana kukawa kumepuliziwa dawa kwenye basi ambalo wanalazimishwa wapande. 

Kitendo hicho kimewafanya Simba kugomea kupanda basi walilolazimishwa wabadilishiwe huku wakiweka msisitizo wa kupanda ambalo lilikuwa kwenye ratiba.

Mechi hiyo itaanza saa 2:30 usiku wa leo. 
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment