Writen by
sadataley
2:55 PM
-
0
Comments
Kamanda wa Kikosi cha Usalama
Barabarani, Mohamed Mpinga, akipokea vifaa vya kuzuia vumbi kwa askari
wa usalama barabarani kutoka kwa msamaria mwema, Tahir Othman (kulia)
,aliyejitolea vifaa hivyo ili kusaidia askari kuepukana na vumbi
kuingia kwenye njia ya hewa wawapo katika shughuli zao.Anayeshuhudia
katikati ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad
Masauni .Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Waziri,jijini
Dar es Salaam.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama
Barabarani, Mohamed Mpinga, akionyesha kwa waandishi wa habari jinsi ya
kuvaa kifaa cha kuzuia vumbi kwa askari wa usalama barabarani
alivyopokea kutoka kwa msamaria mwema,Tahir Othman(hayupo pichani)
,aliyejitolea vifaa hivyo ili kusaidia askari kuepukana na vumbi
kuingia kwenye njia ya hewa wawapo katika shughuli zao.Kushoto ni Naibu
Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mwenyekiti wa
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni.
Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Waziri, jijini Dar es
Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama
Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, akiangalia jinsi ya kuvaa kifaa cha
kuzuia vumbi kwa askari kutoka kwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama
Barabarani, Mohamed Mpinga, ambae pia ni Katibu Mtendaji wa baraza
hilo.Vifaa hivyo vilitolewa na msamaria mwema,Tahir Othman (hayupo
pichani).Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Waziri,jijini
Dar es Salaam.
Chanzo: mjengwablog
No comments
Post a Comment